Basi la New Force lililopata ajali
Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe John Makuri Imori, amesema ajali hiyo imetokea leo Juni 21, 2023, majira ya saa 8:30 mchana, baada ya dereva wa basi hilo kutaka kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari na kupoteza mwelekeo na kutumbukia kwenye mtaro.
"Taarifa za awali ni kwamba basi hilo lilikuwa linatoka Dar es Salaam, dereva alitaka ku-overtake lori likapoteza ueleko na kugonga daraja na kuingia mtaraoni, waliofariki mpaka sasa ni wanaume wanne na mtoto mmoja anayekadiriwa kuwa na miaka nane," amesema Kamanda Imori