Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Wanasheria walimdangaya waziri'-Jaji Mihayo

Jumatatu , 5th Jun , 2023

Jaji msitaafu na Kamishina wa viapo Thomas Mihayo amewataka watendaji wenye taaluma ya sheria walioko kwenye sekta ya umma kutuliza akili katika kufanya maamuzi na ushauri kwa viongozi wakuu hasa katika masuala ya kimikataba hususani katika kipindi hiki ambacho Taifa linaita wawekezaji.

Jaji msitaafu na Kamishina wa viapo Thomas Mihayo

Mstaafu Jaji Thomas Mihayo ametoa rai hiyo kufuatia mwendelezo wa ufatiliaji wa sakata hili linaloonesha kufatiliwa zaidi na wawekezaji ambapo akipitia hukumu ya kesi iliyohusu kampuni kutoruhusu muunganiko wa kampuni mbili katika uwekezaji wa saruji kati ya kampuni ya Tanga cement na Scancerm ambao hadi sasa umeonesha kuvunjwa kwa utawala wa sheria.

Amesema zipo dalili za wazi kwamba wanasheria wa wizara walitoa taarifa zisizo sawa kwa waziri wa Uwekezaji viwanda na Biashara hali iliyopelekea kuzua utata wa kisheria usio zingatia amri ya mahakama.

Aidha Jaji mstaafu Thomas Mihayo amesisitiza kuwa kwa sasa kutofuata amri za mahakama kwenye masuala ya kibiashara kunaweza kuligharimu Taifa kufuatia baadhi ya watendaji wake kuuza miiko.

Utakumbuka hivi karibuni Kampuni ya saruji ya Chalinze Cement, ilifungua kesi katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam, ili kumtaka Wakala wa Usajili Biashara na Leseni (BRELA), kuirudisha mara moja kampuni hiyo katika daftari la kampuni zilizosajiliwa na kutambulika kisheria nchini.

Kesi hiyo namba 113, ya Mwaka 2023 imefunguliwa na Chalinze Cement kupitia kwa Mkurungenzi Mkuu wake Mohamed Hussein Bahdera.

Itakumbukwa, baada ya vuguvugu la mida mrefu kuhusu madai ya BRELA kuifuta kampuni hiyo, hivi karibuni Serikali kupitia Wizara ya Uwekezaji Viwanda na Biashara ilithibitisha kufutwa kwa Kampuni ya Chalinze Cement, kwa madai kuwa nyaraka zake zimegundulika kuwa za uongo wakati wa usajili na Wanahisa wa kampuni hiyo hawatambuliki.

Taarifa hiyo ilitolewa, Machi mwaka huu na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji, Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa akijibu hoja za wabunge wakati akihitimisha mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Hata hivyo, katika mkutano wa wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita, Wakili Melchisedeki Lutema, amesema sakata hilo lilianza mara tu baada ya uamuzi wa Mahakama ya Kibiashara ya Septemba 23, 2022 juu ya kuungana au kutokuungana kwa makampuni ya saruji ya Twiga na Tanga, yalieleza wazi kuwa yamezuia kuungana kwa makampuni hayo na hayakutoa muda maalumu wa kuisha kwa uamuzi huo.

Aliongeza kuwa, katika mazingira hayo Chalinze Cement walijitokeza kupinga muunganiko huo ili kulinda maslahi ya walaji na mazingira ya usawa wa soko.
Akizungumzia kufutwa kwa kampuni ya Chalinze Sementi, wakili huyo alieleza kuwa wameshangazwa na utaratibu uliotumika kwa kuwa wateja wake hawakupewa taarifa na sababu za kufutwa kwake.

HABARI ZAIDI

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma