
Maonesho ya mwaka huu ambayo yamevutia Wajasiliamali zaidi 1500 kutoka Nchi zote saba (7) Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudani na Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo ambapo kati wajasiriamali hao, asilimia 75 ni wanawake, yamesheheni bidhaa mbalimbali za asili kutoka nchi husika zikiongozwa na kauli mbiu ya maonesho haya “Nunua Bidhaa za Afrika Mashariki kwa Uchumi Stahimilivu na Endelevu”
Maonesho haya yanalenga kutoa fursa kwa Wajasiliamali kuonesha huduma na bidhaa mbalimbali wanazozalisha na kubadilishana uzoefu, ujuzi na taarifa na wajasiriamali wenzao katika Jumuiya, sambamba na kukuza wigo wa masoko mapya. Kwa upande wa wajisiliamali wa Tanzania miongoni mwa bidhaa na huduma wanazozionesha ni pamoja na mavazi ya asili, bidhaa za kilimo zilizoongezewa thamani, mashine za kuzalisha bidhaa mbalimbali, madawa ya asili, vito vya dhamani na madini, utalii, na bidhaa za ngozi kama vile viatu, mabegi na mikoba.