
Taarifa hiyo imetolewa leo Desemba 2, 2019, na Meneja Miradi wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Emmanuel Nyalali, wakati akitoa ripoti ya soko kwa juma lililoishia Novemba 29, 2019.
Aidha Nyalali amesema kuwa mpaka sasa thamani ya hatifungani zilizoorodheshwa sokoni hapo, zimefikia trilioni 10.40, ambazo ni sawa na hatifungani za Serikali zenye thamani ya Shilingi trilioni 10.225, na hatifungani zilizotolewa na taasisi za kifedha za Tanzania na za Kikanda zenye thamani ya Shilingi bilioni 176.