Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

NGOs zenye wafadhili zatakiwa TAKUKURU

Ijumaa , 14th Sep , 2018

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa nchini (TAKUKURU), imezitaka kampuni na taasisi zisizo za kiserikali (NGOs) ambazo zinawafadhili mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi, kuwasilisha taarifa zao za misaada ya kifedha kutoka kwa wafadhili wao kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Julius Mbungo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Naibu Mkurugenzi wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Julius amesema "sisi kama taasisi ya kupambana na rushwa tutawafikia, na kama kuna ubadhirifu umefanyika basi wenye hizo NGO's waje kwetu wajisalimishe”

Katika hatua nyingine, taasisi hiyo imetangaza kumtafuta mwenyekiti wa kamati ya usajili wa klabu ya Simba, Zakaria Hanspope ili kujibu tuhuma za udanganyifu wa taarifa kwa Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA) juu ya udanganyifu ununuzi wa nyasi bandia kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa Simba uliopo Bunju, ambapo kwa mujibu Hanspope alinunua kwa dola za kimarekani 40,577 huku bei halisi ni zaidi ya Dola za Kimarekani laki 1.

“Tumekuwa tukimtafuta kwa njia wazi, sio siri, lakini raia huyu mwenzetu haonekani sisi tunachomtaka ajitokeze ajibu tuhuma zinazomkabili na sheria zipo zitamlinda kama hana hatia na kama ana hatia sheria zitafata mkondo wake” , alioongeza Naibu mkurugenzi wa TAKUKURU.

TAKUKURU kwa sasa iko chini ya mkurugenzi mpya ambapo Septemba 6 mwaka huu, Rais Magufuli alimteua Kamishina wa Polisi, Diwani Athumani kuwa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU akishika nafasi ya aliyekuwa mkurugenzi wa taasisi hiyo Kamishina wa Polisi, Valentino Mlowola ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Septemba 12 Rais Magufuli alimuapisha CP Diwani Athumani kuwa mkurugenzi mpya wa TAKUKURU ambapo alimpatia maagizo mbalimbali ikiwemo kupambana kikamilifu na Rushwa na kushughulika na NGOs ambazo zinaendesha shughuli zake kinyume na usajili wao.

Mtazame hapa chini Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Brigedia Jenerali John Julius Mbungo akielezea zaidi..

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali