Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Namna ya kushiriki tuzo za Tehama (ICT Awards2021)

Ijumaa , 27th Aug , 2021

Kuelekea Tuzo za Tehama Tanzania, Mkurugenzi wa Tume ya Tehama Tanzania, Samson Mwela, amesema lengo la tuzo hizo ni kuibua na kukuza vipaji vya wabunifu wa tehama nchini ili kutengeneza taifa la kidijitali.

Mkurugenzi wa Tume ya Tehama Tanzania, Samson Mwela (aliyesimama) akitoa mafunzo kwa Wanahabari na Watangazaji wa East Africa Television na East Africa Radio.

Mwela ameyasema hayo leo Agosti 27, 2021 wakati akitoa mafunzo kwa Wanahabari na Watangazaji wa East Africa Television na East Africa Radio juu ya kazi mbalimbali zinazofanywa na tume hiyo ikiwemo Tuzo za Tehama Tanzania (ICT Awards 2021).

''Kwenye hizi tuzo sio tu tunaangalia wasomi au taasisi ambazo tayari zimeshafanikiwa, tutawafikia wabunifu wengi chipukizi ndio maana tuna vipengele takribani 18 tu kuwatambua wote pamoja na kuzikuza kazi zao ambao kwa namna moja zimeleta suluhu ya changamoto nyingi kwenye jamii'', amesema.

Mkurugenzi wa Tume ya Tehama Tanzania, Samson Mwela (aliyesimama) akitoa mafunzo kwa Wanahabari na Watangazaji wa East Africa Television na East Africa Radio.

Aidha ameeleza kuwa kwasasa zoezi linaloendelea ni watanzania wenyewe kupendekeza majina ya watu au kampuni za watoaji wa huduma bora wa Tehama nchini, kupitia tovuti ya tume https://www.ictc.go.tz/ na litamalizika Septemba 10, na kuanzia Septemba 11 hadi 18 waliopendekezwa watajaza fomu maalum wakieleza nini wamefanya kisha utaratibu wa kuwapigia kura utatolewa.

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi wa Tume ya Tehama Tanzania, Samson Mwela na Wanahabari na Watangazaji wa East Africa Television na East Africa Radio.

Kupitia kituo kilichozinduliwa cha Soft Centre watanzania wabunifu wa tehama wanaendelea kusajiliwa ili watambulike na kazi zao zitambulike ikiwemo kupewa nguvu ya kufikisha mbali zaidi kazi zao, hivyo umetolewa wito watu wachangamkie fursa hiyo.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali