
Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt Pindi Chana
Balozi Dkt Pindi akizungumza jijini Arusha wakati akizindua Bodi ya nne ya Wakala wa Huduma za Misitu nchini TFS,amesema kwa sasa satelite inaonyesha kuwa kipindi hiki si rafiki cha kuchoma mioto kutokana na kuwepo kwa upepo mwingi.
Amesema wapo baadhi ya wananchi wanavamia maeneo ya hifadhi na kufanya shughuli ambazo haziruhusiwi hali inayopelekea kuharibika kwa misitu ambayo ndiyo rasilimali muhimu hapa nchini.
"hivi karibuni baadhi ya wafugaji na wakulima wamekuwa wakiingia katika maeneo ya misitu yaliyohifadhiwa kinyume cha taratibu na kulisha mifugo pamoja na kufanya shughuli za kilimo na kuchoma mkaa katika maeneo hayo jambo hili tulikatae kwa dhati kabisa "Alisema Dkt Chana