Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Makamu wa Rais azungumzia jinsi ya kukuza Uchumi

Jumatano , 25th Mei , 2022

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango amesema eneo huru la kibiashara barani Afrika ni fursa kubwa kwa nchi za bara hilo katika kukuza uchumi na maendeleo.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa majadiliano maalum ya viongozi wakuu wa nchi za Afrika yalioshirikisha wadau na marafiki wa nchi za Afrika kutoka mataifa mengine, majadiliano yaliofanyika katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani unaoendelea Davos nchini Uswisi.
 
Amesema katika kutumia fursa hizo nchi za Afrika zinapaswa kupunguza vikwazo mbalimbali ikiwemo vya kikodi katika ufanyaji biashara pamoja na kuimarisha miundombinu itakayorahisisha biashara hizo katika eneo hilo huru.
 
Ameongeza kwamba ni muhimu kuwekeza katika teknolojia itakayorahisisha kufanya biashara na malipo mbalimbali pamoja na kufanya ubia na sekta binafsi, mashirika ya kimataifa na mataifa mengine ili kuongeza uzalishaji katika viwanda.
 
Makamu wa Rais amesema Tanzania inaendelea kuhakikisha wananchi wanaelewa fursa zilizopo katika eneo huru la biashara barani Afrika pamoja na kuimarisha sekta ya uwekezaji kwa kuingia ubia na wadau mbalimbali ndani na nje ya bara la Afrika ili kuweza kufanya biashara katika ukanda huo huru kwa tija zaidi.
 
Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ameshiriki katika mjadala uliohusu ufufuaji uchumi pamoja na hatua zinazoweza kuchukuliwa katika kurejesha amani na mtangamano duniani ambapo viongozi hao wamejadili namna ya kushirikiana katika kukabiliana kutatua matatizo ya kisiasa yanayopelekea vita na migogoro.
 
Aidha Makamu wa Rais amesema ni muhimu dunia inapokabiliana na changamoto kama vita kutosahau changamoto zingine ikiwemo upungufu wa chakula pamoja na kuhakikisha Afrika inashirikishwa katika maamuzi mbalimbali ya dunia. Amesema Afrika ina fursa kubwa ya kuchangia katika kuleta amani na suluhisho la upatikanaji wa chakula kama itaungana na mataifa mengine kwa kutumia rasilimali zilizopo.
 
Makamu wa Rais Makamu wa Rais yupo Davos nchini Uswisi kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani unaoshirikisha wakuu wa nchi, wakuu wa taasisi na mashirika ya kimataifa pamoja pamoja na wafanyabiashara.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu