Moussa Camara Golikipa mpya raia wa Guinea alibeba matumaini makubwa ya Wana Msimbazi kwa kupata Mlinda Mlango ambaye anauwezo wa kucheza mpira kwa miguu yake. Katika michezo miwili mfululizo nyota huyo amefanya makosa ambaye yameigharimu klabu ya Simba alama 5 ambazo zinaweza kuwa alama muhimu kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu ambao timu hiyo ya mtaa wa Msimbazi Karikaoo imeutafuta kwa misimu mitatu mfululizo bila mafanikio.

20 Oct . 2024

Harry Kane Mshambuliaji wa Bayern Munich jana alifunga goli tatu hat-trick dhidi ya Stuttgat na kufikisha idadi ya hat-trick Sita tangu ajiunge na Bavarians kutokea Tottenham Hotspurs ya Uingereza. Kane anashikilia rekodi ya kuwa Mchezaji mwenye asili ya Uingereza aliyefunga goli nyingi zaidi kwenye ligi kuu nchini Ujerumani mbele ya Kevin Keegan, Jude Bellingham na Tony Woodcock.

20 Oct . 2024

Yanga SC imeshinda mchezo wa Dabi jana kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa kwa ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Wapinzani wao wa jadi timu ya Simba. Yanga ilicheza kwa heshima kubwa kwa kufahamu Simba SC ingekuja kwa nia ya kushambulia kuanzia dakika ya kwanza mchezo kutokana na matokeo ya nyuma dhidi ya Wapinzani wao. Ubora wa Yanga ni mkubwa sana na hii inajidhihirisha kutokana na kuchukua ubingwa mara tatu mfululizo huku ikiwa inatafuta ubingwa wake wa nne kama itafanikiwa kuutetea ubingwa wa ligi msimu huu wa 2024-2025. Ushidni wa jana ni wa nne mfululizo mbele ya Watani wao wa jadi na majirani zao mitaa ya Karikoo Simba SC, Simba imebadilika chini ya Kocha Fadlu Davies lakini bado haijawa timu kamili ambayo inayoweza kubishana na Yanga kutokana na uzoefu wa Yanga kucheza akitimu na utofauti wa madaraja ya mchezaji mmojammoja.

20 Oct . 2024

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akipambana na vijana wa Shule ya Sekondari Kijitonyama.

18 Oct . 2024

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

18 Oct . 2024

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhandisi Hamad Masauni akisikiliza taarifa ya mradi

18 Oct . 2024