
Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Moremi Marwa
Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba Mosi, 2021, wakati yeye na timu yake walipotembelea kwenye ofisi za Makampuni ya IPP Media, za magazeti ya The Guardian, East Africa Television na East Africa Radio, ITV na Radio One pamoja na Capital TV na Capital Radio, kwa lengo la kujifunza na kuona namna vyombo hivyo vinavyoendesha shughuli zake.
Mbali na hayo Moremi akauhakikishia uongozi wa makampuni ya IPP kwamba, kupitia Soko la Hisa la Dar es Salaam watahakikisha wanafanya kazi kwa ukaribu na Makampuni ya IPP Media, kwa lengo la kuhakikisha elimu ya masoko na mitaji ndani ya soko hilo inatolewa na kuwafikia wananchi walio wengi zaidi.