Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Dkt. Nchemba afanya ziara soko la Kariakoo

Jumatano , 3rd Aug , 2022

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amefanya ziara ya kushtukiza soko la Kariakoo na kuagiza  mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutatua changamoto mbalimbali za wafanyabiashara wa Soko hilo ili kuchochea biashara katika soko

Dkt. Nchemba ametoa maagizo hayo baada ya kufanya ziara ya ghafla katika Soko hilo akiambatana na Naibu Spika Na Mbunge wa Ilala Mhe. Mussa Azan Zungu, Mkuu wa Wiaya ya Ilala Bw. Ng’wilabuzu Ludigija na Uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA

Wafanyabiashara wa Soko la Kariakoo walieleza changamoto zao mbalimbali zinazowakabili ikiwemo madai ya kushuka kwa biashara ya Nje kutokana na ukaguzi wa mara kwa mara unaofanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa wafanyabishara wa kigeni, ukaguzi ambao walidai si rafiki.

Walisema kuwa wafanyabiashara kutoka nje wanasumbuliwa kwa kudaiwa kuwa risiti wanazopewa na wafanyabiashara baada ya kununua bidhaa hazikuwa sahihi na kuzuiwa mizigo yao hali inayosababisha usumbufu kwa wageni na kumwomba Mheshimiwa Waziri Nchemba aingilie kati ili kufufua biashara katika Soko hilo.

Aidha, Wafanyabiashara hao waliiomba Serikali iongeze kiwango cha mfanyabiashara kusajiliwa kuwa mlipakodi wa VAT kutoka shilingi milioni 100 hadi shilingi milioni 500 ili kusisimua biashara zao na kuongeza mzunguko wa fedha utakaowasaidia kukua na kuwa wafanyabiashara wakubwa.

Ili kupunguza changamoto za kodi na ukusanyaji wa mapato ya Serikali, wafanyabishara hao walipendekeza kodi zote ziwe zinatozwa bandarini wakati mizigo inapoingia nchini na kuacha biashara katika Soko la Kariakoo iendelee bila bughudha za masuala ya kodi.

Aidha, Wafanyabiashara hao waliwalalamikia baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wasio waaminifu wanaotumia mwanya wa makosa yanayofanywa na baadhi ya wafanybiashara kudai rushwa na kuikosesha Serikali mapato.

Naibu Spika na Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azan Zungu alimwomba Mbeshimiwa Waziri Nchemba, kuwachukulia hatua kali watumishi hao wasiowaaminifu wanaotumia nafasi zao kujinufaisha kwa kudai na kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara.

Aidha, Mhe. Zungu aliishauri Serikali ipunguze kiwango cha kodi ya mapato (VAT) ili kuwawezesha wafanyabiashara kulipa kodi husika kwa urahisi na hiari zaidi hatua ambayo itakuza biashara na faida kwa wafanyabiashara nchini.

Akijibu hoja za wafanyabiashara hao waliokuwa wakimshangilia mara kwa mara, Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, aliiagiza TRA kukutana na wafanyabiashara hao na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili.

Alisema kuwa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameelekeza mazingira ya kufanyiabiashara kwa wafanyabiashara nchini yaboreshwe ili kundi hilo liweze kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi na kukuza ajira.

Aliahidi kuwa katika mwaka wa Fedha ujao wa 2023/2024 kutakuwa na mabadiliko makubwa ya kikodi ikiwemo kupunguza VAT na kuja na utaraibu mzuri utakaohamasisha na kukuza biashara nchini.

Aidha, aliahidi kuwa Serikali itaongeza kiwango cha masharti ya wafanyabiashara wanaostahili kusajiliwa kwenye VAT kutoka kiwango cha sasa cha na VAT cha shilingi milioni 100 na kuwekwa kiwango kipya mwaka mpya wa bajeti utakapofika kwa sababu kiwango hicho cha sasa ni cha chini ikilinganishwa na ukubwa wa biashara zinazofanyika. 

Dkt. Nchemba aliiagiza pia TRA kutozuia mizigo ya wafanyabiashara wa kigeni wanaonunua bidhaa zao katika Soko la Kariakoo na kuwataka washughulike na wafanyabiashara wasiowaaminifu waliotenda makosa husika kwa kuwa mifumo ya ndani ya nchi haiwahusu wafanyabiashara hao.

Katika hatua nyingine, aliwataka wafanyabiashara hao kuwa waaminifu na kufanyabiashara kwa kufuata misingi mizuri iliyowekwa ikiwemo kutoa risiti halalali zinazolingana na bidhaa walizouza ili kuepuka usumbufu.

Aidha, Dkt. Nchemba aliwaonya watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wasiowaaminifu wanaojihusisha na vitendo vya kudai na kupokea rushwa na kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao na kuwataka wafanyabiashara hao kutoa taarifa ya watumishi wa namna hiyo wanaoikosesha Serikali mapato.

Kwa upande wake Kamishna wa Kodi za Ndani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, aliyemwakilisha Kamishna Mkuu katika ziara hiyo ya kushtukiza, Bw. Herbert Kabyemela, aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizowasilishwa na wafanyabiashara hao na kubainisha kuwa tatizo kubwa linaloikabili Mamlaka hiyo ni suala la ukosefu wa uaminifu wa wafanyabiashara hususan katika kutoa risiti zinazolingana na bidhaa wanazouza.

Dkt. Nchemba aliwaahidi wafanyabiashara hao kwamba atarejea tena sokoni hapo hivi karibuni kusikiliza kero na changamoto zao na kwamba mkutano huo alioufanya utaleta mabadiliko ili Soko hilo la Kariakoo liendelee kuchangia mapato ya Serikali na uchumi wa wafanyabiashara kwa ujumla
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu