Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bei ya mafuta yapaa

Jumanne , 7th Aug , 2018

Bei za mafuta ya Petroli, Dizeli na mafuta ya meli visiwani Zanzibar zimeshuka huku bei ya mafuta ya taa ikitajwa kupanda kwa asilimia 4 mwezi Agosti na kufikia kuuzwa shilingi 1,854 kwa lita.

Kituo cha kutolea huduma ya mafuta

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha uhusiano kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji Zanzibar (ZURA), Khuzaimat Bakar na wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari na kusema bei hizo mpya zitaanza kutumika rasmi leo Agosti 07, 2018 katika vituo vyote vya kuuzia mafuta visiwani Zanzibar.

"Bei ya reja reja mafuta ya taa kwa mwezi wa Agosti, 2018 imepanda kwa shilingi 77 kwa lita kutoka shilingi 1,777 kwa lita mwezi Julai, 2018 hadi shilingi 1,854 katika mwezi wa Agosti sawa na asilimia 4. Mafuta ya Petrol kwa bei ya reja reja kwa mwezi Agosti yameshuka kwa shilingi 25 kwa lita kutoka shilingi 2,435 ya mwezi Julai, 2018 hadi shillingi 2,410 kwa lita mwezi Agosti, 2018 ambayo sawa na asilimia 1", amesema Khuzaimat.

Pamoja na hayo, Khuzaimat ameendelea kufafanua kuwa "bei ya reja reja ya dizeli kwa mwezi Agosti imeshuka kwa shilingi 35 kwa lita kutoka shilingi 2,430 ya mwezi Julai hadi shilingi 2395 sawa na asilimia 1.4".

Mbali na bei hizo, pia Khuzaimat amesema bei ya mafuta ya meli yameshuka kwa mwezi Agosti kwa shilingi 36 kwa lita kutoka shilingi 2,259 kwa lita katika mwezi Julai, 2018, hadi shilingi 2,222 katika mwezi Agosti sawa na asilimia
1.5.

Kushuka kwa baadhi ya bei hizo kunatokana mabadiliko ya mauzo ya mafuta hayo katika soko la dunia.

Bei ya Mafuta ya Petroli katika soko la dunia kwa mwezi wa Julai, 2018 imeshuka kwa shilingi 13 sawa na asilimia 1, bei ya mafuta ya Dizeli ikishuka kwa shilingi 33 sawa na asilimia 2.5, bei ya mafuta ya meli kushuka kwa shilingi 33 sawa na asilimia 2.5  huku bei ya mafuta ya taa yakiwa yamepanda kwa shilingi 107 sawa na asilimia 9.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto