22 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za mauaji
Jeshi la polisi mkoa wa Mara nchini Tanzania kwa kushirikiana na raia wema limefanikiwa kuwakamata watu 22 kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya kuwachinja na kuwanyonga wanawake saba kutoka baadhi ya vijiji vya mwambao wa Ziwa Victoria.