MAKUNDI 5 YAPENYA FAINALI DANCE 100%
Baada ya mpambano wa kukata na shoka, hatimaye makundi matano ya kudansi Team ya shamba, Best Boys, Team Makorokocho, The WD na The winners wamefanikiwa kuingia fainali ya mashindano makubwa ya Dance 100% (2015), baada ya kufanikiwa kujivunia alama zaidi katika mashindano hayo yaliyofanyika Don Bosco Oysterbay jijini Dar es Salaam siku ya juzi (Jumamosi).
Ushindani mkali ulionyeshwa na washiriki wote juu ya jukwaa la kisasa, ubunifu katika mitindo ya kucheza na mavazi kwa makundi hayo ukiwa ni kiburudisho kingine kikubwa kwa umati mkubwa uliohudhuria mashindano hayo.

