TFF yasitisha ziara ya timu ya Taifa ya vijana

Timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U15) ikikabidhiwa bendera ya Taifa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel katika hosteli za TFF zilizopo Karume jijini Dar es salaam.

Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 15 inarejea jijini Dar es salaam baada ya ziara yake ukanda wa Afrika Mashariki kusitishwa kufuatia kukosekana kwa fedha ya kuihudumia baada ya TRA kufungia akauti za shirikisho la soka nchini TFF.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS