Watford watawala tuzo za EPL mwezi Disemba 2015

Kocha mkuu wa Watford Quique Sánchez Flores(kushoto)akiwa na nyota Odion Ighalo(kulia)kwenye picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa tuzo za kocha na mchezaji bora wa EPL kwa mwezi disemba mwaka jana.

Mshambuliaji wa klabu ya Watford Odion Ighalo na kocha wake Quique Sanchez Flores wametajwa kuwa mchezaji na kocha bora wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza kwa mwezi disemba.

Ighalo raia wa Nigeria aliifungia mabao matano mwezi disemba na kuiwezesha Watford kuzishinda klabu za Norwich City, Liverpool, Sunderland huku ikitoa sare na Chelsea na kupoteza mechi moja pekee dhidi ya Totenham Hotspurs.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS