92% ya watu duniani wanaishi kwenye hewa chafuzi
Takwimu mpya za shirika la afya duniani (WHO) kuhusu ubora wa hewa, zimethibitisha kwamba asilimia 92% ya watu duniani wanaishi katika maeneo ambapo viwango vya ubora wa hewa ni vidogo kupita kiasi cha ukomo kilichowekwa na shirika hilo.