Arusha walalamikia ubovu miundombinu ya maji
Katika kuelekea msimu wa mvua baadhi ya wakazi wa mtaa wa Kambi ya Fisi, kata ya Ngarenaro mkoani Arusha wameuomba uongozi wa serikali ya mkoa, kuchukua tahadhari za mapema katika kuandaa njia za mitaro ya maji taka ili kuepukana na adha ya mafuriko.