CTI yataka Tanzania imiliki viwanda vya madini
Shirikisho la Wenye Viwanda nchini (CTI) limesisitiza haja ya Tanzania kuwa na viwanda vyake vya kuchenjua na kuongezea thamani bidhaa za madini na kuacha kusafirisha nje madini ghafi kwani uwezo wa kufanya hivyo upo.