Tanzania yaahidi kuisaidia Serikali mpya Burundi
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa amesema Tanzania itaendelea kuisaidia Burundi ili ifanikiwe katika adhma yake ya kutaka kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kama ilivyoombwa na aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Pierre Nkurunziza wakati wa uhai wake.

