Simba kutwaa ubingwa kwa staili ya Liverpool?
Klabu ya Simba SC inaweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara (VPL) hii leo iwapo Azam FC itashindwa kupata alama tatu dhidi ya Biashara United kwenye mechi itakayopigwa jioni katika uwanja wa Karume mkoani Mara.

