Tuesday , 5th May , 2026

Leo kwenye usiku wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya macho yote ni kwenye mchezo wa awamu ya pili ya nusu fainali  Klabu ya Arsenal ikiikaribisha Atletico Madrid katika uwanja wa Emirates.

Victor Gyokeres na Julian Alvarez

Baada ya sare ya 1-1 kule Madrid wiki iliyopita, timu zote zinahitaji ushindi ili kufika fainali ya Budapest nchini Hungary.

‎Arsenal huenda ikawakosa Martin Ødegaard na Kai Havertz ambao walikosa mazoezi ya mwisho, huku Jurriën Timber na Mikel Merino wakiwa nje kwa majeraha huku

Atletico, Antoine Griezmann na Julián Alvarez wanatarajiwa kuongoza mashambulizi, huku beki Clément Lenglet akirejea kikosini.