Hans Flick Kocha wa Barcelona
Flick ametoa kauli hiyo baada ya kikosi chake kupoteza mechi ya ligi dhidi ya Girona, ambayo ilimalizika kwa ushindi wa 2-1, tukio lililoongeza ushindani mkali katika mbio za ubingwa msimu huu wa 2025/26.
Kocha huyo raia wa Ujerumani pia ameitaja Real Madrid, akisema imekuwa ikipata manufaa katika baadhi ya mechi zake, tofauti na Barcelona, ambayo imekabiliwa na matokeo mabaya yanayohusiana, kwa kiasi kikubwa, na maamuzi mabovu ya waamuzi.
"Nimechoka kudhani kwamba hali hii ni ya kawaida. Penalti zinazotoa urahisi katika mechi za Real Madrid. Uamuzi wa mashaka katika mechi za wapinzani. Mifumo inayojirudia mara zote inaonekana kupendelea upande mmoja” Flick
Matokeo ya mechi dhidi ya Girona yameendelea kuiweka Barcelona katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa LaLiga, ikiwa na pointi 58, huku Real Madrid ikiongoza ligi ikiwa na pointi 60 baada ya timu zote kucheza mechi 24






