Tuesday , 2nd Dec , 2025

“Tunapita katika wakati mgumu.. lakini ninakuhakikishia mama Naomi Mwakyoma Kaihula, Chama chako hakitakengeuka. Yale uliyoyaamini, uliyoyapigania hadi mwisho wa maisha yako tutayaendeleza na kuyaheshimu.”

 

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, ametoa kauli hiyo yenye hisia wakati wa msiba wa Mama Naomi, aliyewahi kuwa Mbunge na mwanachama imara wa CHADEMA, pia mama mzazi wa msanii maarufu wa hiphop King GK (Gwamaka Kaihula).

Mama Naomi alifahamika kwa msimamo wake usioyumba katika haki, usawa na demokrasia.