Saturday , 21st Jun , 2025

Katika hotuba yake kwenye Tamasha la Utamaduni la Bulabo linalofanyika Kanda ya Ziwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

ametoa wito mzito kwa waganga wa kienyeji kuacha tabia ya kutumia ramli chonganishi ambazo zimekuwa chanzo cha migogoro, mfarakano na vurugu hasa wakati wa chaguzi.

 

Tamasha hilo, ambalo linahusisha makabila mbalimbali ya Kanda ya Ziwa, linaendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza utamaduni wa Kitanzania na kuhimiza maelewano.  

 

Kauli ya Rais Samia imepokelewa kama wito wa kitaifa kwa ajili ya kudumisha utulivu na mshikamano kuelekea uchaguzi mkuu ujao.