Friday , 23rd May , 2025

Msanii wa kizazi kipya Kusah amefunguka kuwa hana kabisa mipango ya kuachana na mke wake AAunty Ezekiel kwasababu ana kila kitu ambacho yeye anakitaka,mbali na hiyo pia ameweka wazi kuwa kwasasa ni rasmi wawili hao ni Mke na Mume

Akifanya interview na kipindi cha East Africa TV Friday Night Live Msanii Kusah amesema...... "Mimi nikiingia sehemu mpaka Umati ukajua nipo ujue nina malengo napo halafu pia naangalia nimebakiza kitu gani nini? nina watoto zaidi ya mmoja nina mwanamke ana akili na ananiheshimu hata kama tukipishana nikitoka hapo nikienda sehemu nyingine tutapishana tu''

"Kwahiyo mimi kwa malengo yangu sijui kama tutaachana, tayari tumeoana niko huru kuongea popote na ndoa tulifungia nyumbani kwetu Bumbuli mkoani Tanga''