
Picha ya mafuriko DRC
Hayo yameelezwa na msimamizi wa wilaya ya Fizi katika mkoa wa Kivu Kusini Samy Kalodji, ambaye ameeleza kwamba mafuriko hayo yameathiri kijiji cha Kasaba ambako taarifa zinaonesha kwamba zaidi ya watu 100 wamekufa.
Mafuriko hayo yanashuhudiwa kwenye eneo hilo katika wakati ambapo mashambulizi ya waasi wa M23 yameongezeka katika eneo hilo la Mashariki tangu mwanzoni mwa mwaka huu.
Maelfu ya watu waliuwawa katika kipindi cha miezi miwili ya mwanzo mwa mwaka huu, kufuatia mapigano hayo.