
Kocha wa Barcelona Hansi Flick
Licha ya kutofautiana mitizamo miezi michache iliyopita kuhusu hatma yake inatajwa kuwa uamuzi huo umefanywa na rais Joan Laporta na bodi ya wakurugenzi.
Flick alisaini mkataba wa miaka miwili baada ya kuwasili Catalonia, lakini katika wiki za hivi karibuni kumekuwa na mazungumzo kuhusu yeye kuongeza mkataba.
Barcelona na Flick wamefikia makubaliano ya kuongeza mkataba kwa msimu mmoja zaidi pamoja na wakufunzi wake, watapokea nyongeza ya mishahara kama sehemu ya mkataba huu mpya, ambao utatangazwa mwisho wa msimu huu.