Friday , 14th Jun , 2024

Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia katika mtaa wa Buganda kata ya Mkolani jijini Mwanza baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuteketea kwa moto wakati wakiwa ndani peke yao.

Nyumba iliyoteketea kwa moto

Wakizungumza kwa huzuni wazazi wa watoto hao wamesema walikuwa hawajarudi nyumbani wakati moto unaanza kuwaka, na wakati wanarudi walishtushwa kuona moto mkubwa unawaka na kuteketeza nyumba na mali zote, na kupelekea vifo vya watoto hao.

Kwa upande wa majiarani na mashuhuda wa tukio hilo wamesema wakati wanafika moto ulikuwa unawaka kwa kasi kubwa na kufanikiwa kumuokoa mtoto mmoja,  huku wakishindwa kuingia ndani kumuokoa mtoto mwingine aliyekuwemo. 

Kamanda wa Jeshi la zimamoto  na uokoaji mkoa wa Mwanza Kamila Labani, anasema pamoja na jitihada za uokozi walizofanya lakini tayari mtoto mmoja amefariki huku mwingine akifariki akiwa hospitali na chanzo cha moto ni mtoto mmojawapo kuwasha moto kwenye godoro.