![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2024/05/02/BASSHE WEEEB.jpg?itok=eBBiioW2×tamp=1714642421)
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 2, 2024, wakati akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa mwaka 2024/2025.
Amesema kutokana na hali hiyo, Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa asilimia 124 ikilinganishwa na utoshelevu wa asilimia 114 mwaka 2022/2023, aidha, utoshelevu wa chakula unatarajiwa kufikia asilimia 130 ifikapo mwaka 2025.