
Mshukiwa amezuiliwa baada ya kupigwa risasi huko Sindelfingen, polisi katika mji wa karibu wa Ludwigsburg wamethibitisha taarifa hizo
Kikosi hicho hapo awali kiliandika kwenye Twitter: "Kwa sasa kuna operesheni ya polisi kwenye eneo la kiwanda. Polisi na waokoaji wako kazini na kwamba hakuna hatari kwa idadi ya watu ambao wanaendelea na kazi
Mercedes Benz imethibitisha kuwa tukio limetokea huko Sindelfingen na inawasiliana na mamlaka.
Kampuni hiyo ilisema katika taarifa yake kwamba wamewasiliana na mamlaka na kueleza kwa kina ukweli wa tukio hilo na kwamba Usalama wa wafanyikazi ndio kipaumbele chao.