Wednesday , 13th Jul , 2022

Watu watatu wa familia moja akiwemo Kaka, Dada na mtoto mdogo wamefariki dunia usiku wa kuamkia leo Julai 13, 2022, baada ya kugongwa na gari katika barabara ya East Africa, hali iliyopelekea mamia ya wakazi wa Kata ya Muriet jijini Arusha kufunga barabara wakinishikiza iwekwe alama.

Baadhi ya wananchi wa Kata ya Muriet waliofunga barabara,

Mwenyekiti wa Kata ya Muriet Emmanuel Sanale, ameomba Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Arusha kufanya jitihada za haraka za kurekebisha barabara hiyo kwa kuwa ni nyembamba.

Kwa upande wake mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Mrisho Gambo, mara baada ya kufika katika eneo hilo ameahidi kufuatilia na kutatua changamoto ya barabara hiyo Ili kupunguza madhara ya mara kwa mara ya vifo vinavyotokea.