Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TPA yapokea magari 4397 kwa pamoja

Tuesday , 10th May , 2022

Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) imevunja rekodi kwa kupokea meli yenye magari 4397 ambayo yametoka nchini Japan na hivyo kuwa meli ambayo imepokelewa bandari ya Dar es salaam ikiwa na magari mengi zaidi. Awali, bandari ya Dar es salaam ilipokea meli yenye magari 4041 mwezi April 2022.

Sehemu ya magari 4397 yakiwa tayari yameshushwa bandarini

Mamlaka ya Bandari nchini Tanzania (TPA) imesema kuwa meli ya Meridian Ace ambayo imetia nanga katika bandari ya Dar es Salaam ikiwa na jumla ya magari 4397 kwasasa ndiyo meli ya kwanza kushusha magari mengi kwa pamoja katika historia ya bandari hiyo na TPA.

"Hii meli ya meridian ace imevunja rekodi kwa kuingiza magari 4397 kwa wakati mmoja, imevunja rekodi ya meli tuliyoipokea mwezi Aprili mwaka huu ambayo ilikuwa na magari 4041. Imetoka moja kwa moja nchini Japan lakini ilipita Singapore kabla ya kufika Tanzania"- Nicodemus Mushi, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano - TPA.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa mamlaka ya bandari (TPA) Bw. Nicodemus Mushi amefafanua kwamba asilimia 23 ya magari hayo yanabakia nchini Tanzania huku asilimia 77 yakiwa ni ya mataifa nchi jirani. Ameongeza kuwa kupokea magari mengi kiasi hiki ni matokeo ya kuaminika kwa huduma za bandari ya Dar es salaam na kuwashukuru wadau kwa kuitumia bandari hiyo.

"Katika magari haya, 23% yanabakia nchini hapa na 77% ya magari haya yanakwenda nchi jirani ya Zambia, Malawi, Rwanda, Burundi, na Congo DR. Hii inamanisha kwamba wadau wetu wameendelea kuamini huduma za bandari ya Dar es salaam, lakini pia usalama, uharaka wa huduma na uaminifu" - Nicodemus Mushi, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano - TPA

 

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90