Monday , 9th Aug , 2021

Mchezaji wa klabu ya Simba, Jonas Mkude amerejea kambini kuungana na wachezaji wenzake baada ya kusimamishwa na timu yake kwa muda usiojulikana na sababu kubwa ikielezwa ni masuala ya kinidhamu.

Picha ya Mchezaji Jonas Mkude

Kiungo mkabaji huyo ameonekana na wachezaji ambao tayari wamewasili kambini tayari kwa maandalizi ya msimu mpya wa mashindano.

Kocha wa timu hiyo Didier Gomes aliagiza wachezaji wote kuingia kambi wiki hii ili kuanza maandalizi ya msimu ujao ambao inaelezwa kuwa kambi yao itawekwa nchini Morocco.