
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe, akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Mwenyekiti huyo wa CHADEMA na wenzake walifikishwa Mahakamani mapema leo Agosti 6, 2021, baada ya hapo jana kesi hiyo kushindwa kuendeshwa kufuatia matatizo ya kimtandao yaliyohusisha usikilizaji kesi kwa video conference baina ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Gereza la Ukonga.