
Chelsea wakishangilia ubingwa
Huu ni ubingwa wao wa pili katika historia ya klabu hiyo ambapo ubingwa wa kwanza walitwaa mwaka 2012 kwa kuwafunga Bayern Munich.
Rekodi mbalimbali zilizowekwa
Mlinzi wa kati wa Chelsea raia wa Brazil Thiago Silva ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa tano kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa misimu miwili mfululizo akiwa na klabu tofauti wengine Marcel Desailly, Paulo Sousa, Samuel Eto’o na Álvaro Morata.
Mlinzi wa kati wa Chelsea Thiago Silva
Thiago Silva pia ndio mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi (miaka 36) kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ndani ya kikosi cha Chelsea akiivunja rekodi ya Claude Makélélé dhidi ya Manchester United mwaka 2008 alipocheza akiwa na miaka 35 na siku 93.
Kocha Pep Guardiola amepoteza fainali mbili za mashindano katika historia yake ya kufundisha soka tangu mwaka 2008. Alipoteza fainali ya Copa del Rey msimu wa 2010-11 akiwa na Barcelona na sasa amepoteza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea.
Kocha wa Man City Pep Guardiola
Wakati kocha wa Chelsea Thomas Tuchel ametwaa ubingwa katika fainali yake ya pili baada ya kupoteza fainali ya msimu uliopita 2019-20 dhidi ya Bayern akiwa na PSG.
Kocha wa Chelsea Thomas Tuchel
Pia Thomas Tuchel amekuwa kocha wa pili kumfunga Pep Guardiola katika mechi tatu mfululizo za mashindano yote akitanguliwa na kocha wa Liverpool Jürgen Klopp ambaye alifanya hivyo mwaka 2018.