Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga yatangaza Kaimu Katibu Mkuu mpya

Friday , 20th Nov , 2020

UongozI wa Klabu ya Yanga, leo Novemba 20 umemtangaza Haji Mfikirwa kuwa Kaimu Katibu Mkuu wa klabu hiyo, akichukua nafasi ya wakili Simon Patrick ambaye amesimamishwa kutokana na tuhuma za kuihujumu timu.

Haji Mfikirwa Kaimu Katibu Mkuu mpya wa Yanga SC

Mfikirwa ametangazwa na Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Frederick Mwakalebela mbele ya waandishi wa habari. Katika utambulisho huo Mwakalebela amesema Kamati ya Utendaji inamuamini Haji na ataweza kuipeleka mbele klabu hiyo kutokana na uwezo mkubwa alionao.

Haji Mfikirwa anachukua nafasi ya Patrick Simon ambaye alisimamishwa kazi Novemba 18, kutokana na tuhuma za kuihujumu Yanga, ikiwemo kufanya vikao vya siri na viongozi wa mahasimu wao wa soka hapa nchini.

Lakini pia katika mkutano huo na wanahabari Mwakalebela ameliomba Shirikisho la Soka nchini (TFF) kuzifanyia kazi kesi zao walizo ziwasilisha ikiwemo ile ya Ramadhani Kabwili, pamoja na ile inayohusu juu ya uhalali wa mkataba wa Bernard Morrison na klabu ya Simba.

Aidha Yanga wameomba kesi ya mkataba wa Morrison na klabu ya Simba isikilizwe kabla ya dirisha dogo la usajili halijafunguliwa Disemba 15, 2020 kwani kuna ujanja unaweza kufanyika wa kubadilisha mkataba huo.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90