Tuesday , 6th Oct , 2020

Meneja wa kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani  cha Ubungo, Mahela Nkhama Chilosa, amesema katika kipindi cha mwezi mmoja ujao kituo hicho kinaweza kuhamishiwa Mbezi kama mipango ya serijkali itakuwa imekamilika ikiwemo kukamilika miundo mbinu ya kituo kipya cha Mbezi.

Meneja wa kituo cha mabasi cha Ubungo, Mahela Nkhama Chilosa.

Akiongea na EATV, Chilosa amesema awali serikali ilishasema kwamba mwisho wa matumizi ya kituo cha mabasi Ubungo ni mwezi wa kumi lakini kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya vitu ndio sababu inayofanya kituo hicho kisihame kwa wakati. 

''Hapa kwa sasa tupo lakini sidhani kama katika kipindi cha mwezi mmoja ujao tutakuwepo na nafikiri hata hizi kampeni nazo zimechangia maana viongozi wengi wapo huko'', amesema Chilosa.

Ameongeza, hata baadhi ya mabasi yameshaanza kuondoka ndani ya kituo na kutumia maeneo yao ya kuegesha mabasi hayo kama ndio kituo cha kupanda na kushusha abiria.