
Novak Djokovic
Djokovic ambaye alishinda taji la Ufaransa mnamo 2016, analenga kuwa mtu wa kwanza katika enzi za uwazi kushinda kila Grand Slams mara mbili.
Raia huyo wa Serbia ameweka rekodi mpya katika michuano hiyo kwa kufuzu hatua ya robo fainali kwa mwaka wa 11 mfululizo.
Nyota namba moja wa tenisi Duniani kwa wanaume Novak Djokovic
Katika hatua hiyo ya robo fainali Djokovic, atakabiliana na Pablo Carreno Busta raia wa Hispania.
Katika mchezo mwingine Stefanos Tsitsipas wa Ugiriki, alifika robo fainali yake ya kwanza kwa ushindi dhidi ya Grigor Dimitrov raia wa Bulgaria.