Bernard Membe akirejesha fomu
Makabidhiano hayo yamefanyika Ofisi ya ACT Wazalendo Magomeni, jijini Dar es salaam ambapo amekabidhi fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa ACT Wazalendo Ndugu Joran Bashange.
Membe ambaye kauli mbiu yake alitaja kuwa ni Kazi na Bata, alikubali kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo, kwa kile alichodai kwamba huo ni wakati muafaka kwake wa kushiriki mazungumzo na vyama vingine ili waweze kusimamisha mgombea mmoja.
Julai 16 wakati akizungumza na wanachama wa ACT Wazalendo, alieleza ni kwa namna gani alifedheheshwa, baada ya kufukuzwa uanachama na CCM, "Mimi nimefukuzwa tena kwa aibu na kutukanwa na vijana ambao ningeweza kuwazaa, na sikutenda kosa lolote hata mbele ya Mungu, kosa nililofanya ni la kugombea Urais 2015".




