
Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson na mchumbwa wake Carrie Symonds
Mtoto huyo ambaye amezaliwa siku ya Jumatano ametangazwa kupewa jina hilo jana Mei 2,2020, huku jina hilo ni ishara ya heshima kwenda kwa madaktari waliomtibu Waziri ugonjwa wa Corona wakati alipoumwa ugonjwa huo.
Akizungumza kwenye akaunti binafsi ya mtandao wa Instagram mchumba wa Waziri wa Uingereza Carrie Symonds amesema "Jina la Wilfred ni baada ya babu wa Boris, Lawrie ni baada ya Babu yangu, na Nicholas ni kwa heshima ya Madaktari waliomsaidia kumtibu Corona Boris ambao ni Dr. Nick Prince na Nick Hart"
Waziri huyo anatarajia kurejea kazini Jumatatu ya Mei 4,2020 baada ya kuwa kiongozi wa kwanza mkubwa duniani kutangazwa kuwa ana virusi vya ugonjwa wa Corona mnamo mwezi Machi.
Chanzo : CNN