
Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako
Taarifa hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa mtandao huo Davis Komba, kwa kile alichokieleza kuwa Serikali inapaswa kuzingatia suala hilo kama ambavyo Mataifa mengine yalivyoamua kufunga shule baada ya kugundua visa vya waathirika wa ugonjwa huo.
"Wizara ya Elimu ione vyema kusimamisha masomo kwa Shule, Vyuo na Vyuo Vikuu kama hatua ya tahadhari kwa umma, kwani wanafunzi wapo kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa" imeeleza taarifa hiyo.