Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga
Anna Henga ameandika hayo leo Machi 10, 2020, Kupitia ukurasa wake wa Twitter, ikiwa imepita siku moja tu tangu timu ya Yanga, ilipoipa kichapo cha goli timu ya Simba, katika mchuano wake wa mpira wa watani wa jadi.
"Hongera sana mashabiki wa Yanga, hata hivyo naomba lugha inayotumika isiwe ya kudhalilisha jinsia ya kike!, unaposema Simba kaolewa au Yanga kaolewa unamaanisha kuwa kuolewa ni kushindwa (kufungwa), kwa kawaida anayeolewa ni Mwanamke! maana yake ni nini? #Aminiausawa" ameandika Anna Henga.
