
Picha ya marehemu Kobe Bryant enzi hizo akicheza kwenye timu yake ya LA Lakers
Katika hafla hiyo walijitokeza mastaa mbalimbali wakiwemo Kanye West, Kim Kardashian, Beyonce, Snoop Dogg , Alicia Keys, Jennifer Lopez, Alex Rodriguez, Michael Jordan, Steph na Ayesha Curry.
Picha ya mke wa Kobe Bryant aitwaye Vanessa Bryant
Sasa moja ya vitu vilivyotokea kwenye shughuli hiyo ni staa wa Pop duniani Beyonce kukataa kupigwa picha alipokuwa anaimba wimbo wa XO na Halo kama heshima ya mwisho kwa Kobe Bryant.
Picha ya msanii Beyonce akiwa anaimba katika kumbukumbu ya maisha ya Kobe Bryant
Mkongwe wa mchezo wa Basketball Michael Jordan, kumwaga machozi hadharani wakati akielezea ukaribu aliokuwa nao na Kobe Bryant.
Mkongwe wa mchezo wa Basketball Michael Jordan akitokwa na machozi
Pia katika uwanja huo wa Staples Center, ndipo mahali walipoagwa na kutolewa heshima za mwisho kwa mkali wa muziki wa pop Michael Jackson na rapa Nipsey Hussle.
Uwanja wa Staples Center mahali ambapo shughuli hiyo imefanyika
Wawili hao tayari walishazikwa siku ya Februari 7,2020 katika makaburi ya Pacific view memorial park jijini California.