
Zitto Kabwe amesema kifo cha Mama huyo ni moja ya vifo, ambavyo vimegusa idadi kubwa ya Watanzania, kutokana na namna ambavyo Erick Kabendera alikuwa akiishi vizuri na watu.
Zitto Kabwe ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye mazishi ya Mama Mzazi wa Erick Kabendera, yaliyofanya jana Januari 6, 2020, katika Kijiji cha Kashenge, Kata ya Katoma Bukoba Vijiji, mkoani Kagera.
"Katika kesi mbili za mwisho ambazo Erick alikuwa mahakamani, Mama alikuja, tulimlaumu Dada yake Rose kwanini alikuwa anamleta Mama, kumbe mama alikuwa anamuaga Mwanae" amesema Zitto.
Mama wa Erick Kabendera alifariki Dunia siku ya Disemba 31, 2019, katika hospitali bya Amana iliyoko jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
#VIDEO Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), @absakibanda akizungumzia jinsi alivyoguswa na kifo cha Mama Mzazi wa Erick Kabendera, Verdiana Mujwahuzi katika mazishi ya Mama huyo kijijini Kashenge Bukoba Vijijini
Taqzama :-https://t.co/upTOejFW61 pic.twitter.com/JJaVXXwPcv
— East Africa Radio (@earadiofm) January 7, 2020