
Mfungwa Mussa Msola akiwa chii ya Ulinzi wa Polisi
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Khamis Issah, amesema mfungwa huyo amedumu nje ya msamaha kwa saa nane tu baada ya hapo akaenda kufanya tukio la uhalifu kwa kuvunja, moja ya nyumba za wageni mkoani Njombe.
"Ni saa nane zimepita mtuhumiwa ambaye aliachiwa kwa msamaha wa Rais,alijikuta anaenda kuvunja gesti ya Nyang'ano, lakini wananchi walimdhibiti." amesema Kamanda Issah.
Akizungumza baada ya kutiwa nguvuni na Jeshi la Polisi, Msolwa amesema kuwa alipitiwa licha ya kuwa aliahidi kubadilika, lakini ameshindwa.