Tuesday , 23rd Sep , 2014

Ziara ya msanii wa muziki Akon nchini Kenya, inatarajiwa kuwa na manufaa pia kwa wasanii wa muziki wa nchini humo kwani kati ya mambo aliyozungumza na kiongozi mkuu wa nchi hiyo, ni kuanzisha mpango wa kuinua vipaji vya wasanii hawa.

msanii wa muziki nchini Senegal Akon akiwa na rais Uhuru Kenyatta wa Kenya

Katika kuhakikisha utekelezaji wa hili, vilevile mradi wa Umeme ambao ndio mpango mkubwa, msanii huyu anatarajiwa kurejea tena nchini Kenya kabla ya kuisha kwa mwaka huu, ili kuhakikisha kuwa mambo haya yanafanikishwa vizuri.

Akiwa nchini Kenya, mbali na kukutana na Rais Kenyatta Ikulu, msanii huyu mkubwa alipata nafasi ya kukutana na wadau wengine, akiwepo msanii wa muziki Jaguar ambaye muunganiko huu waweza kuzaa chochote kisanaa.