
Waziri Lugola ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Kigoma alipotembelea kambi ya Wakimbizi Nduta, iliyopo wilayani Kibondo mkoani humo akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Burundi.
Waziri Lugola amesema kuwa "wakimbizi wa Burundi wanaoishi Tanzania, wanalelewa vizuri sana na mpango wa Serikali ni kuwarejesha nyumbani kwao Burundi, kwa kuwa sasa kuna amani."
Aidha akieleza nia hiyo Waziri Lugola amesema Serikali katika kila wiki itakuwa ikiwarudisha wakimbizi ili 2000 mpaka pale watakapoisha.