
Hayo yameelezwa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoani wa Kagera Dkt. John Mwombeki baada ya kupokea msaada vifaa mbalimbali ambavyo hutumiwa na watu wanaojitokeza kujitolea damu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salum Mstaafu Mstapha Kijuu amewahimiza wananchi katika mkoa wa kagera wajenge utamaduni wa kujitolea damu ili waweze kuokoa maisha ya wagonjwa ambao wakati mwingine hupoteza maisha kutokana na sababu ya tatizo la upungufu wa damu katika hospitali hiyo
Msaada wa vifaa vinavyotumika wakati wa kutoa damu umetolewa na wadau mbalimbali kwa ajili ya kukiimarisha kitengo cha damu safi na salama cha hospitali hiyo ili kiweze kukusanya damu nyingi itayokidhi mahitaji ya wagonjwa