Monday , 12th Sep , 2016

Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA kimetuma salaam za pole kwa wananchi wote walioathirika na tetemeko la ardhi katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Mwanza, Tabora na kwingine, na kusababisha vifo vya watu 16 majeruhi na uharibifu wa mali.

Nembo la CHADEMA

Akitoa salamu za pole kupitia taarifa hii Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano CHADEMA bwana Tumaini Makene amesema chama kinatoa wito kwa watanzania wote katika maeneo yaliyopatwa na tetemeko hilo na wengine kutoka nje ya sehemu hizo, kuguswa na tukio hilo na kuwiwa kuwasaidia waathirika wa tukio hilo katika wakati huu mgumu wa kukabiliana na athari zilizotokana na janga hilo.

Viongozi wa chama katika ngazi mbalimbali, wabunge, madiwani na wanachama wote wa CHADEMA wataungana na kusaidiana kwa kila hali na wote walioguswa na tukio hilo katika wakati huu mgumu wa kupoteza ndugu, jamaa, marafiki, kusitiri miili ya marehemu, kuuguza majeruhi na kupata hifadhi mbalimbali kwa waliopoteza mali na makazi.